Blogger Widgets Blogger Widgets

Monday, March 17, 2014

HIVI NDIVYO PRODUCER MSWAKI ALIVYOIJIBU BONGO5 MEDIA BAADA YA KUSEMA KUWA ANATAFUTA #KIKI.


Mambo yalianza baada ya Bongo5 media kuandika makala ambayo ilikuwa inaongelea Producer Mahiri ambaye sauti yake inafanana na marehemu Albert mangwair kiasi kwamba kabla ya mauti kumkuta marehemu alishawahi kumkataza kwamba anaomba asitumie style yake i mean ya marehemu(ngwair) na ikumbukwe baada ya kifo cha albert mangwair Mswaki alitoa track ikiwa kama kuombeleza msiba wa ngwair na track hiyo illitwa "Open letter" sasa mambo yalianza Pale ambapo Mswaki alitangaza kuwa anataka kufanya project yenye jina #keepingNgweaAliveProject na kuamua kwenda kwa mama yake na marehemu kuomba baraka zake na ndipo alipozua mjadala kwenye media mbalimbali Tz...

Hapo juu ni makala ambayo Bongo5 ilijaribu kuchambua na ikajipa majibu bila kumshirikisha producer Mswaki kwa kusema anatafuta kiki, Hivyo Mswaki kwa kutumia  nguvu ya umma ( internet ) akaamua kutumia busara zake kujibu hivi;

Really? #Obsessed? #KutafutaKiki? #Bongo5 naomba nieleweke hivi...
1.Kwanza kabisa nyie kama chombo cha habari mlikuwa na haki kimsingi ya kunitafuta mimi mwenyewe na kuniuliza kama mlikuwa mnataka kujua kuhusiana na hii project,kuliko KUANDIKA na KUJIPA MAJIBU pasipo kuwa na taarifa za kutosha
2.Mnasema kwamba mimi najaribu au nataka kuchukua character ya marehemu Albert,I CAN NEVER BE ARBERT hata siku moja kwa sababu muziki ni sehemu ndogo sana ya maisha au tabia ya mtu.
3.Mi naamini kila mtu anaweza kumuenzi marehemu kwa nafasi yake hata kama ni kidogo sana,kama mnanifatilia kwa makini sijawahi kusema kwamba mimi ni ZAIDI ya marehemu Albert.
4.Hiki kitu nilikuwa nakifanya kwa nia njema na nilikuwa naamini ni moja ya njia ya kumfanya Albert aendelee kuishi kimziki kwa upande mwingine.
5.Kuweza kufanya kama marehemu ni moja ya sababu tu iliyonipelekea kufanya #keepingNgweaAliveProject,lakini kimsingi project ilikuwa inamuhusu Ngwea moja kwa moja kuanzia kitu alichokiimba na naamna navyoimba mimi ndo maana nikaenda kuwaona wazazi wake ili nao waweze kupata mwanga wa project nzima.
Je kuna wasanii wangapi mashuhuri waliofanya vitu vikubwa sana na wakasahaulika kabisa KIMUZIKI?nilikuwa najaribu kuwa mfano kwa hii project kwa kuleta muamko katika jamii wa kuwambuka watu mashuhuli waliotutangulia KWA CHOCHOTE KIDOGO ULICHONACHO. Ahsante

No comments: